Jarida la Mapishi

Mchuzi wa samaki

Mchuzi wa samaki | Jarida la Mapishi
  • Maandalizi
    -
  • Kupika
    Dakika 30
  • Walaji
    4

Mchuzi wa samaki, ni kitoweo kitamu ambacho hupikwa kwa kutumia samaki wabichi, vitunguu maji, tui la nazi, ukwaju, pamoja na viungo vya aina mbalimbali. Mchuzi huu wafaa kula pamoja na wali, chapati au mkate. Fuata hatua zifuatazo, ili ujifunze jinsi ya kupika mchuzi huu wa samaki.

Ingredients

    Directions

    Step1

    Chukua sufuria kubwa lenye mafuta ya kupikia na uliweke kwenye jiko lenye moto wa wastani, kisha acha mafuta yapate moto. Weka vitunguu maji kwenye hilo sufuria, kisha kaanga huku ukikoroga mara kwa mara kwa muda wa dakika 5, au hadi utakapo ona vimeiva.

    Step2

    Weka vitunguu swaumu, kisha kaanga huku ukikoroga mara kwa mara kwa muda wa dakika 1.

    Step3

    Chukua mashine ya kusaga (blender). Weka kwenye hiyo mashine ya kusaga, mbegu za giligilani pamoja na binzari nyembamba, kisha saga hadi utakapo ona mchanganyiko huo umesagika vizuri.

    Step4

    Weka binzari ya manjano, kisha saga hadi utakapo ona mchanganyiko huo wote umechanganyika vizuri.

    Step5

    Ondoa mchanganyiko huo kwenye mashine ya kusaga na uweke kwenye sufuria lenye vitunguu, kisha kaanga huku ukikoroga mara kwa mara kwa muda wa dakika 2.

    Step6

    Mimina maji pamoja na tui la nazi, kisha weka moto mkubwa na uache ichemke huku ukikoroga mara kwa mara.

    Step7

    Ukiona imeanza kuchemka, punguza moto na uweke moto wa wastani, kisha acha iendelee kuchemka kwa muda wa dakika 5.

    Step8

    Weka Tamarind Paste pamoja na chumvi halafu koroga vizuri, kisha acha ichemke kwa muda wa dakika 1.

    Step9

    Weka vipande vya minofu ya samaki, halafu acha ichemke kwa muda wa dakika 10 mpaka 15, au hadi utakapo ona vimeiva, kisha epua na upakue kwenye chombo safi, tayari kwa kula.

    Unaweza Pia Kusoma Hizi

    Leave a Review

    Your email address will not be published. Required fields are marked *


    The reCAPTCHA verification period has expired. Please reload the page.