Jarida la Mapishi

Mchuzi wa kuku

Mchuzi wa kuku | Jarida la Mapishi
  • Maandalizi
    -
  • Kupika
    Dakika 55
  • Walaji
    4

Mchuzi wa kuku, ni pishi lenye ladha tamu ambalo hupikwa kwa kutumia nyama ya kuku, mtindi, vitunguu maji, nyanya, pamoja na viungo vya aina mbalimbali. Fuata hatua zifuatazo, ili ujifunze jinsi ya kupika, mchuzi huu wa kuku.

Ingredients

    Directions

    Step1

    Chukua mashine ya kusaga (blender). Weka kwenye hiyo mashine ya kusaga, vitunguu swaumu, tangawizi, pamoja na vitunguu maji, kisha saga hadi utakapo ona mchanganyiko huo umesagika vizuri na kuwa laini. Ondoa mchanganyiko huo kwenye mashine ya kusaga, na uweke pembeni kwenye kontena.

    Step2

    Weka kwenye hiyo hiyo mashine ya kusaga, nyanya pamoja na majani ya giligilani, kisha saga hadi utakapo ona mchanganyiko huo umesagika vizuri na kuwa laini. Ondoa mchanganyiko huo kwenye mashine ya kusaga na uweke pembeni kwenye kontena jingine.

    Step3

    Chukua sufuria kubwa lenye mafuta ya kupikia na uliweke kwenye jiko lenye moto wa wastani, kisha acha mafuta yapate moto. Weka kwenye hilo sufuria, majani ya mbei, iliki, pamoja na mdalasini, kisha kaanga huku ukikoroga mara kwa mara kwa muda wa sekunde 30.

    Step4

    Weka mchanganyiko wa vitunguu maji ulio usaga, kisha kaanga huku ukikoroga mara kwa mara kwa muda wa dakika 7, au hadi utakapo ona mchanganyiko huo umebadilika rangi na kuwa na rangi ya kahawia.

    Step5

    Weka mchanganyiko wa nyanya ulio usaga, kisha pika mchanganyiko huo huku ukikoroga mara mwa mara kwa muda wa dakika 7, au hadi utakapo ona mchuzi umekuwa mzito.

    Step6

    Weka mbegu za giligilani, binzari nyembamba, garam masala, binzari ya manjano, chumvi, pamoja pilipili manga, kisha koroga vizuri.

    Step7

    Mimina mtindi huku ukikoroga, kisha pika mchanganyiko huo huku ukikoroga mara kwa mara, hadi utakapo ona mtindi umechanganyika vyema pamoja na mchanganyiko wa viungo.

    Step8

    Weka vipande vya nyama ya kuku, kisha pika mchanganyiko huo huku ukikoroga mara kwa mara kwa muda wa dakika 5, au hadi utakapo ona vipande hivyo vya nyama ya kuku vimebadilika rangi na kuwa na rangi ya kahawia.

    Step9

    Mimina maji halafu koroga vizuri, kisha funika sufuria na uache ichemke kwa muda wa dakika 5.

    Step10

    Punguza moto na uweke moto wa wastani, halafu acha iendelee kuchemka huku ukivigeuza vipande vya nyama ya kuku mara kwa mara kwa muda wa dakika 30, au hadi utakapo ona vimeiva na mchuzi umekuwa mzito, kisha epua na upakue kwenye chombo safi, tayari kwa kula.

    Conclusion

    Kabla ya kutumia mtindi huo, hakikisha unaupiga piga vizuri ukiwa kwenye bakuli kwa kutumia kijiko kama unavyo yapiga piga mayai unapotaka kuyakaanga, hadi utakapo ona mtindi umekuwa laini na hauna mabonge mabonge.

    Unaweza Pia Kusoma Hizi

    Leave a Review

    Your email address will not be published. Required fields are marked *


    The reCAPTCHA verification period has expired. Please reload the page.