-
MaandaliziDakika 40
-
KupikaDakika 20
-
Walaji12
Muffins za ulezi na matunda damu, ni muffins ambazo hupikwa kwa kutumia unga wa ulezi, unga wa ngano, pamoja na matunda damu yaliyo katwa katwa. Muffins hizi zafaa sana kula kama kifungua kinywa wakati wa asubuhi. Fuata hatua zifuatazo, ili ujifunze jinsi ya kupika muffins hizi za ulezi na matunda damu.
Ingredients
Directions
Chukua bakuli kubwa. Weka ndani ya hilo bakuli, unga wa ulezi, unga wa ngano ambao hauja kobolewa, chumvi, light brown sugar, pamoja na baking soda, kisha changanya vizuri.
Weka mayai, almond milk, mafuta ya nazi, pamoja na matunda damu, kisha changanya vizuri kwa kutumia mashine ya kuchanganyia (mixer), hadi utakapo ona mchanganyiko huo umechanganyika vyema na kuwa laini.
Chukua sufuria la kuoka muffins (muffins pan), lenye matundu 12 ya muffins, na uweke ndani ya hayo matundu karatasi za kuokea muffin (muffin papers). Chukua bakuli lenye mchanganyiko ulio changanya na mashine ya kuchanganyia, na umimine mchanganyiko huo kwenye sufuria la kuoka muffins.
Washa jiko la kuoka, na uweke joto la nyuzi 175° C, kisha acha jiko lipate moto. Jiko likishapata moto, weka sufuria la kuoka muffins ndani ya hilo jiko, na uoke kwa muda wa dakika 20, au hadi utakapo ona muffins zimeiva na kuwa na rangi ya kahawia.
Muffins zikisha iva, ziondoe kwenye jiko la kuoka, kisha ziweke pembeni ili zipoe, zikiwa bado ndani ya sufuria la kuoka muffins. Muffins zikishapoa, unaweza kuzitoa ndani ya sufuria la kuoka muffins, tayari kwa kula.
Leave a Review