Jarida la Mapishi

Achari ya maembe mabichi

Achari ya maembe mabichi | Jarida la Mapishi
  • Maandalizi
    -
  • Kupika
    Dakika 1
  • Walaji
    1

Achari ya maembe mabichi, ni achari ya ambayo hutengenezwa kwa kutumia maembe mabichi, chumvi, sukari, vitunguu vya kijani, pamoja na viungo vya aina mbalimbali. Achari hii yafaa kutumika kwenye chakula cha ina yoyote. Fuata hatua zifuatazo, ili ujifunze jinsi ya kutengeneza achari hii ya maembe mabichi.

Ingredients

    Directions

    Step1

    Chukua mashine ya kusaga (blender). Weka kwenye hiyo mashine ya kusaga, maembe, tangawizi, vitunguu vya kijani, majani ya mvuje, pamoja na chumvi, kisha saga hadi utakapo ona mchanganyiko huo umesagika vizuri na kuwa laini. Ondoa mchanganyiko huo kwenye mashine ya kusaga na uweke pembeni kwenye kontena.

    Step2

    Weka sukari ndani ya hilo kontena, kisha changanya vizuri.

    Step3

    Chukua sufuria dogo lenye mafuta ya kupikia na uliweke kwenye jiko lenye moto wa wastani, kisha acha mafuta yapate moto. Weka kwenye hilo sufuria, mbegu za haradali pamoja na mbegu za uwatu, kisha kaanga huku ukikoroga mara kwa mara kwa muda wa sekunde 30. Epua mchanganyiko huu na umimine kwenye kontena lenye mchanganyiko wa maembe, kisha changanya vizuri.

    Step4

    Weka achari hiyo kwenye chombo safi chenye mfuniko, kisha hifadhi kwenye friji.

    Unaweza Pia Kusoma Hizi

    Leave a Review

    Your email address will not be published. Required fields are marked *


    The reCAPTCHA verification period has expired. Please reload the page.