Jarida la Mapishi

Vimanda vya viazi vya kuponda

Vimanda vya viazi vya kuponda | Jarida la Mapishi
  • Maandalizi
    -
  • Kupika
    Dakika 35
  • Walaji
    4

Vimanda vya viazi vya kuponda, ni kitafunio kitamu ambacho hupikwa kwa kutumia kiazi mviringo kilicho chemshwa na kupondwa, mayai, vitunguu maji, pamoja na viungo. Kitafunio hiki chafaa kula kama kifungua kinywa wakati wa asubuhi, pamoja na kinywaji chochote ukipendacho. Fuata hatua zifuatazo, ili ujifunze jinsi ya kupika vimanda hivi vya viazi vya kuponda.

Ingredients

    Directions

    Step1

    Chukua sufuria dogo. Weka kwenye hilo sufuria kiazi mviringo, chumvi kiasi, pamoja na maji, kisha chemsha kwenye jiko lenye moto wa wastani kwa muda wa dakika 20, au hadi utakapo ona kimeiva.

    Step2

    Epua na umwage maji yote yaliyomo kwenye sufuria na kubakiwa na kiazi peke yake, kisha acha kipoe.

    Step3

    Menya maganda ya kiazi hicho, kisha kiponde vizuri.

    Step4

    Chukua kontena la ukubwa wa wastani. Weka ndani ya hilo kontena, kiazi ulichokiponda, mayai, vitunguu maji, ¼ kikombe cha majani ya giligilani, tangawizi, chumvi, pamoja na pilipili manga, kisha changanya vizuri.

    Step5

    Chukua kikaango kikubwa chenye mafuta ya kupikia na ukiweke kwenye jiko lenye moto wa wastani, kisha acha mafuta yapate moto. Weka kwenye hicho kikaango, mchanganyiko wa mayai uliochanganya, kisha funika kikaango na ukaange kwa muda wa dakika 3, au hadi utakapo ona upande wa chini wa mchanganyiko huo umebadilika rangi na kuwa na rangi ya kahawia. (Weka mchanganyiko huo wa mayai kwa awamu 2 mpaka 3)

    Step6

    Nyunyizia ¼ kikombe cha majani ya giligilani yaliyobaki juu ya huo mchanganyiko wa mayai, kisha kandamiza taratibu majani hayo kwa kutumia kijiko cha kukaangia (spatula) ili yashikane vizuri na mchanganyiko wa mayai.

    Step7

    Chukua sahani kubwa. Weka sahani hiyo ndani ya kikaango, kisha pindua kikaango juu chini ili kimanda kipate kigeuka na kuhamia kwenye sahani.

    Step8

    Telezesha kimanda kwenye kikaango, halafu rudisha kikaango kwenye jiko, kisha kaanga upande wa pili wa kimanda hicho kwa muda wa dakika 2, au hadi utakapo ona na upande huo umebadilika rangi na kuwa na rangi ya kahawia.

    Step9

    Kunja kimanda katikati, kisha ondoa kwenye kikaango na ukiweke kwenye sahani, tayari kwa kula. Rudia hatua ya 5 mpaka 9, kwa mchanganyiko wa vimanda uliobaki.

    Unaweza Pia Kusoma Hizi

    Leave a Review

    Your email address will not be published. Required fields are marked *


    The reCAPTCHA verification period has expired. Please reload the page.