Jarida la Mapishi

Pilau ya giligilani na njegere

Pilau ya giligilani na njegere | Jarida la Mapishi
  • Maandalizi
    Dakika 30
  • Kupika
    Dakika 25
  • Walaji
    4

Pilau ya giligilani na njegere, ni chakula kitamu na chenye afya, ambacho hupikwa kwa kutumia mchele, majani ya giligilani, njegere, vitunguu maji, pamoja na viungo vingine vya aina mbalimbali. Chakula hiki chafaa kula pamoja na mchuzi wa kuku, mchuzi wa nyama ya ng’ombe, mchuzi wa samaki, au mchuzi wa maharage. Fuata hatua zifuatazo, ili ujifunze jinsi ya kupika pilau hii ya giligilani na njegere.

Ingredients

    Directions

    Step1

    Chukua kontena la ukubwa wa wastani. Weka maji, kisha roweka mchele ndani ya hilo kontena lenye maji kwa muda wa dakika 30.

    Step2

    Chukua sufuria kubwa lenye mafuta ya kupikia na uliweke kwenye jiko lenye moto wa wastani, kisha acha mafuta yapate moto. Weka kwenye hilo sufuria, binzari nyembamba, madalasini, iliki, pamoja na vitunguu maji, kisha kaanga huku ukikoroga mara kwa mara kwa muda wa dakika 3, au hadi utakapo ona vitunguu vimebadilika rangi na kuwa na rangi ya kahawia.

    Step3

    Ongeza moto na uweke moto mkubwa. Weka vitunguu swaumu, njegere, majani ya giligilani, garam masala, pamoja na chumvi, kisha kaanga huku ukikoroga mara kwa mara kwa muda wa dakika 2.

    Step4

    Weka mchele pamoja na maji uliyotumia kurowekea mchele, halafu koroga vizuri, kisha acha ichemke.

    Step5

    Ukiona imeanza kuchemka, punguza moto na uweke moto mdogo, kisha funika sufuria na uache iendelee kuchemka taratibu kwa muda wa dakika 12 mpaka 15, au hadi utakapo ona wali umeiva na maji yote kwenye sufuria yamekauka. Hakikisha hukorogi kabisa wali wakati unaupika.

    Step6

    Zima jiko, kisha acha pilau itulie kwa muda wa dakika 5, ikiwa bado juu ya jiko. Baada ya dakika 5, pakua pilau kwenye chombo safi, tayari kwa kula.

    Unaweza Pia Kusoma Hizi

    Leave a Review

    Your email address will not be published. Required fields are marked *


    The reCAPTCHA verification period has expired. Please reload the page.