-
Maandalizi-
-
KupikaDakika 40
-
Walaji4
Ingredients
Directions
Chukua sufuria kubwa. Weka kwenye hilo sufuria, spinachi, viazi, maji, pamoja na chumvi, kisha weka ichemke kwenye jiko lenye moto mkubwa.
Ukiona imeanza kuchemka, punguza moto na uweke moto mdogo, kisha funika sufuria na uache iendelee kuchemka kwa muda wa dakika 15 mpaka 20, au hadi utakapo ona viazi vimeiva.
Koroga mboga hizo kwa kasi ili kuvivunja baadhi ya viazi kwa ajili ya kupata mchuzi mzito kama krimu, kisha epua na uweke pembeni.
Chukua sufuria la ukubwa wa wastani lenye mafuta ya kupikia na uliweke kwenye jiko lenye moto wastani, kisha acha mafuta yapate moto. Weka kwenye hilo sufuria, binzari nyembamba pamoja na vitunguu maji, kisha kaanga huku ukikoroga mara kwa mara kwa muda wa dakika 5, au hadi utakapo ona vitunguu maji vimeiva.
Weka tangawizi pamoja na vitunguu swaumu, kisha kaanga huku ukikoroga mara kwa mara, hadi utakapo ona vimebadilika rangi na kuwa na rangi ya kahawia.
Weka nyanya, kisha pika mchanganyiko huo huku ukikoroga mara kwa mara kwa muda wa dakika 5 mpaka 7, au hadi utakapo ona mchuzi umekuwa mzito.
Weka mbegu za giligilani, garam masala, pamoja na binzari ya manjano, kisha endelea kupika mchanganyiko huo huku ukikoroga mara kwa mara kwa muda wa dakika 1 zaidi. Epua mchanganyiko huo na umimine kwenye sufuria lenye mchanganyiko wa spinachi, kisha changanya vizuri.
Funika sufuria hilo, halafu weka ichemke kwenye jiko lenye moto mdogo kwa muda wa dakika 5 mpaka 7, kisha epua na upakue kwenye chombo safi, tayari kwa kula.
Leave a Review