Jarida la Mapishi

Kuku wa spinachi

Kuku wa spinachi | Jarida la Mapishi
  • Maandalizi
    -
  • Kupika
    Dakika 55
  • Walaji
    4

Kuku wa spinachi, ni kitoweo kitamu na rahisi kupika, ambacho hupikwa kwa kutumia nyama ya kuku, spinachi, vitunguu maji, mtindi, pamoja na viungo vya aina mbalimbali. Kitoweo hiki chafaa kula pamoja na wali mweupe, wali wa binzari ya manjano au chapati. Fuata hatua zifuatazo, ili ujifunze jinsi ya kupika kitoweo hiki cha kuku wa spinachi.

Ingredients

    Directions

    Step1

    Chukua kontena kubwa. Weka ndani ya hilo kontena, vipande vya nyama ya kuku, mtindi, tangawizi, vitunguu swaumu, majani ya minti, majani ya uwatu, garam masala, kungumanga, chumvi, pamoja na kijiko 1 cha chakula cha mafuta ya kupikia, kisha changanya vizuri hadi utakapo ona vipande vyote vya nyama ya kuku vimeenea vyema viungo. Funika vizuri kontena hilo, kisha liweke kwenye friji kwa muda wa saa 4 mpaka saa 24.

    Step2

    Chukua sufuria kubwa lenye vijiko 2 vya chakula vya mafuta ya kupikia na uliweke kwenye jiko lenye moto wa wastani, kisha acha mafuta yapate moto. Weka vitunguu maji kwenye hilo sufuria, kisha kaanga huku ukikoroga mara kwa mara kwa muda wa dakika 10 mpaka 12, au hadi utakapo ona vitunguu vimebadilika rangi na kuwa na rangi ya kahawia.

    Step3

    Weka spinachi kisha koroga vizuri. Funika sufuria kisha pika mchanganyiko huo kwa muda wa dakika 5, au hadi utakapo ona spinachi imenyauka. Kumbuka kukoroga mara 1 au 2 wakati unapika.

    Step4

    Ongeza moto na uweke moto mkubwa. Weka mchanganyiko wa kuku, kisha pika mchanganyiko huo huku ukikoroga mara kwa mara kwa muda wa dakika 2 mpaka 3.

    Step5

    Punguza moto na uweke moto wa wastani, kisha endelea kupika mchanganyiko huo huku ukikoroga mara kwa mara kwa muda wa dakika 30, au hadi utakapo ona vipande vya nyama ya kuku vimeiva.

    Step6

    Mimina maziwa halafu koroga vizuri, kisha acha ichemke kwa muda wa dakika 2. Epua na upakue kwenye chombo safi, tayari kwa kula.

    Conclusion

    Kabla ya kutumia mtindi huo, hakikisha unaupiga piga vizuri ukiwa kwenye bakuli kwa kutumia kijiko kama unavyo yapiga piga mayai unapotaka kuyakaanga, hadi utakapo ona mtindi umekuwa laini na hauna mabonge mabonge.

    Unaweza Pia Kusoma Hizi

    Leave a Review

    Your email address will not be published. Required fields are marked *


    The reCAPTCHA verification period has expired. Please reload the page.