Jarida la Mapishi

Kuku wa pichi na nyanya

Kuku wa pichi na nyanya | Jarida la Mapishi
  • Maandalizi
    -
  • Kupika
    Dakika 45
  • Walaji
    4

Kuku wa pichi na nyanya, ni chakula kilicho sheheni ladha ya utamu na uchachu, ambacho hupikwa kwa kutumia nyama ya kuku, pichi, limao, vitunguu maji, nyanya, pamoja na viungo. Kitoweo hiki chafaa kula pamoja na wali au mkate, hasa katika msimu wa kiangazi. Fuata hatua zifuatazo, ili ujifunze jinsi ya kupika kitoweo hiki cha kuku wa pichi na nyanya.

Ingredients

    Directions

    Step1

    Chukua mashine ya kusaga (blender). Weka kwenye hiyo mashine ya kusaga, tangawizi, vitunguu swaumu, pichi, pamoja na nyanya, kisha saga hadi utakapo ona mchanganyiko huo umesagika vizuri na kuwa laini.

    Step2

    Chukua sufuria kubwa lenye mafuta ya kupikia na uliweke kwenye jiko lenye moto wa wastani, kisha acha mafuta yapate moto. Weka vitunguu maji kwenye hilo sufuria, kisha kaanga huku ukikoroga mara kwa mara kwa muda wa dakika 10, au hadi utakapo ona vimebadilika rangi na kuwa na rangi ya kahawia.

    Step3

    Ongeza moto na uweke moto mkubwa. Weka mbegu za giligilani, binzari nyembamba, garam masala, pilipili manga, chumvi, vipande vya nyama ya kuku, pamoja na mchanganyiko wa pichi ulio usaga, kisha pika mchanganyiko huo huku ukikoroga mara kwa mara kwa muda wa dakika 5 mpaka 7.

    Step4

    Punguza moto na uweke moto mdogo, kisha endelea kupika mchanganyiko huo huku ukikoroga mara kwa mara, hadi utakapo ona vipande vya nyama ya kuku vimeiva na mchuzi umekua mzito.

    Step5

    Weka limao pamoja na majani ya giligilani, halafu pika mchanganyiko huo huku ukikoroga mara kwa mara kwa muda wa dakika 5, kisha epua na upakue kwenye chombo safi, tayari kwa kula.

    Unaweza Pia Kusoma Hizi

    Leave a Review

    Your email address will not be published. Required fields are marked *


    The reCAPTCHA verification period has expired. Please reload the page.