Jarida la Mapishi

Maboga ya kusaga

Maboga ya kusaga | Jarida la Mapishi
  • Maandalizi
    -
  • Kupika
    Dakika 35
  • Walaji
    4

Maboga ya kusaga, ni chakula kizuri na chenye afya, ambacho hupikwa kwa kutumia maboga yaliyo sagwa, vitunguu maji, pamoja viungo vya aina mbalimbali. Chakula hiki chafaa kula chenyewe kama kilivyo, au waweza kula pamoja na wali au chapati. Fuata hatua zifutazo ili ujifunze jinsi ya kupika maboga haya ya kusaga.

Ingredients

    Directions

    Step1

    Chukua sufuria kubwa lenye mafuta ya kupikia na uliweke kwenye jiko lenye moto wa wastani, kisha acha mafuta yapate moto. Weka kwenye hilo sufuria, mbegu za shamari, mbegu za uwatu, black seeds, pamoja na vitunguu maji, kisha kaanga huku ukikoroga mara kwa mara kwa muda wa dakika 5 mpaka 6, au hadi utakapo ona vitunguu vimeiva.

    Step2

    Weka tangawizi, kisha koroga vizuri.

    Step3

    Weka maboga, kisha kaanga huku ukikoroga mara kwa mara kwa muda wa dakika 5 mpaka 7.

    Step4

    Weka mbegu za giligilani, binzari ya manjano, pamoja na chumvi, kisha koroga vizuri.

    Step5

    Ongeza moto na uweke moto mkubwa. Mimina maji halafu koroga vizuri, kisha funika sufuria na uache ichemke kwa muda wa dakika 2.

    Step6

    Punguza moto na uweke moto mdogo, kisha acha iendelee kuchemka kwa muda wa dakika 20, au hadi utakapo ona maboga yameiva na kuwa laini.

    Step7

    Chukua mashine ya kusaga (blender). Weka kwenye hiyo mashine ya kusaga, mchanganyiko wa maboga ulio upika, kisha saga hadi utakapo ona mchanganyiko huo umesagika vizuri na kuwa laini. Ondoa mchanganyiko huo kwenye mashine ya kusaga na uweke pembeni kwenye chombo safi, tayari kwa kula.

    Unaweza Pia Kusoma Hizi

    Leave a Review

    Your email address will not be published. Required fields are marked *


    The reCAPTCHA verification period has expired. Please reload the page.