Jarida la Mapishi

Mboga ya karoti, njegere na viazi

Mboga ya karoti, njegere na viazi | Jarida la Mapishi
  • Maandalizi
    -
  • Kupika
    Dakika 20
  • Walaji
    4

Mboga ya karoti, njegere na viazi, ni mboga yenye virutubisho vingi na rahisi kupika, ambayo hupikwa kwa kutumia karoti, njegere, viazi mviringo, pamoja na viungo. Mboga hii yafaa kula kama chakula cha mchana au cha jioni, pamoja na wali au mkate. Fuata hatua zifuatazo, ili ujifunze jinsi ya kupika mboga hii ya karoti, njegere na viazi.

Ingredients

    Directions

    Step1

    Chukua sufuria kubwa lenye mafuta ya kupikia na uliweke kwenye jiko lenye moto wa wastani, kisha acha mafuta yapate moto. Weka kwenye hilo sufuria, binzari nyembamba pamoja na tangawizi, kisha kaanga huku ukikoroga mara kwa mara kwa muda wa dakika 1, au hadi utakapo ona vimebadilika rangi na kuwa na rangi ya kahawia.

    Step2

    Ongeza moto na uweke moto mkubwa. Weka mbegu za giligilani, binzari ya manjano, chumvi, karoti, viazi mviringo pamoja na njegere halafu funika sufuria, kisha pika mchanganyiko huo huku ukikoroga mara kwa mara, hadi utakapo ona umepata moto.

    Step3

    Punguza moto na uweke moto wa wastani. Mimina maji, kisha pika mchanganyiko huo huku ukikoroga mara kwa mara kwa muda wa dakika 10, au hadi utakapo ona viazi vimeiva.

    Step4

    Weka majani ya giligilani, kisha pika mchanganyiko huo huku ukikoroga mara kwa mara kwa muda wa dakika 5.

    Step5

    Weka mango powder pamoja na pilipili manga halafu koroga vizuri, kisha epua na upakue kwenye chombo safi, tayari kwa kula.

    Unaweza Pia Kusoma Hizi

    Leave a Review

    Your email address will not be published. Required fields are marked *


    The reCAPTCHA verification period has expired. Please reload the page.