Jarida la Mapishi

Mboga ya kauliflawa, karoti na maharage machanga

Mboga ya kauliflawa, karoti na maharage machanga | Jarida la Mapishi
  • Maandalizi
    -
  • Kupika
    Dakika 15
  • Walaji
    4

Mboga ya kauliflawa, karoti na maharage machanga, ni mboga tamu na rahisi kupika, ambayo hupikwa kwa kutumia kauliflawa, karoti, maharage machanga, vitunguu maji, pamoja na viungo. Mboga hii yafaa kula pamoja na wali wa binzari ya manjano au chapati. Fuata hatua zifuatazo, ili ujifunze jinsi ya kupika mboga hii ya kauliflawa, karoti na maharage machanga.

Ingredients

    Directions

    Step1

    Chukua sufuria kubwa lenye mafuta ya kupikia na uliweke kwenye jiko lenye moto wa wastani, kisha acha mafuta yapate moto. Weka kwenye hilo sufuria, binzari nyembamba, mbegu za kisibiti, vitunguu maji, pamoja na kijiko 1 cha chakula cha tangawizi, kisha kaanga huku ukikoroga mara kwa mara kwa muda wa dakika 1.

    Step2

    Weka kijiko 1 cha chakula cha tangawizi iliyobaki pamoja na vitunguu swaumu, kisha kaanga huku ukikoroga mara kwa mara kwa muda wa dakika 1.

    Step3

    Weka mbegu za giligilani pamoja na binzari ya manjano, kisha koroga vizuri.

    Step4

    Weka vikombe vya mboga mchanganyiko pamoja na chumvi, kisha kaanga huku ukikoroga mara kwa mara kwa muda wa dakika 5, au hadi utakapo ona mboga hizo zimebadilika rangi na kuwa na rangi ya kahawia.

    Step5

    Weka nyanya, kisha pika mchanganyiko huo huku ukikoroga mara kwa mara kwa muda wa dakika 1.

    Step6

    Funika sufuria, kisha pika mchanganyiko huo kwa muda wa dakika 5, au hadi utakapo ona mboga zimeiva.

    Step7

    Weka white vinegar pamoja na majani ya giligilani, kisha pika mchanganyiko huo huku ukikoroga mara kwa mara kwa muda wa dakika 1.

    Step8

    Weka garam masala halafu koroga vizuri, kisha epua na upakue kwenye chombo safi, tayari kwa kula.

    Unaweza Pia Kusoma Hizi

    Leave a Review

    Your email address will not be published. Required fields are marked *


    The reCAPTCHA verification period has expired. Please reload the page.