Jarida la Mapishi

Mchuzi wa kuku wenye lozi

  • Maandalizi
    -
  • Kupika
    Dakika 45
  • Walaji
    4

Ingredients

    Directions

    Step1

    Chukua mashine ya kusaga (blender). Weka kwenye hiyo mashine ya kusaga, vitunguu maji, unga wa dengu, mdalasini, pamoja na karafuu, kisha saga hadi utakapo ona mchanganyiko huo umesagika vizuri na kuwa laini. Ondoa mchanganyiko huo kwenye mashine ya kusaga na uweke pembeni kwenye kontena.

    Step2

    Weka kwenye hiyo hiyo mashine ya kusaga, tangawizi, vitunguu swaumu, lozi, 1 kijiko cha chakula cha mafuta ya kupikia, pamoja na chumvi, kisha saga hadi utakapo ona mchanganyiko huo umesagika vizuri na kuwa laini.

    Step3

    Chukua kontena kubwa. Weka ndani ya hilo kontena, vipande vya nyama ya kuku pamoja na mchanganyiko wa tangawizi ulio usaga, kisha changanya vizuri hadi utakapo ona vipande vyote vya nyama ya kuku vimeenea vyema viungo. Funika vizuri kontena hilo, kisha liweke kwenye friji kwa muda wa saa 4 mpaka saa 24.

    Step4

    Chukua sufuria kubwa lenye vijiko 2 vya chakula vya mafuta ya kupikia na uliweke kwenye jiko lenye moto wa wastani, kisha acha mafuta yapate moto. Weka vipande vya nyama ya kuku kwenye hilo sufuria, kisha kaanga huku ukikoroga mara kwa mara kwa muda wa dakika 10, au hadi utakapo ona vimebadilika rangi na kuwa na rangi ya kahawia.

    Step5

    Weka mchanganyiko wa vitunguu maji ulio usaga, kisha mimina mtindi taratibu huku ukikoroga.

    Step6

    Punguza moto na uweke moto mdogo, kisha funika sufuria na uache ichemke kwa muda wa dakika 15, au hadi utakapo ona mtindi umekauka. Kumbuka kukoroga mara 1 au 2 wakati inachemka.

    Step7

    Mimina tui la nazi halafu koroga vizuri, kisha funika sufuria na uache iendelee kuchemka kwa muda wa dakika 20 zaidi au hadi utakapo ona vipande vya nyama ya kuku vimeiva, kisha epua na upakue kwenye chombo safi, tayari kwa kula.

    Conclusion

    Kabla ya kutumia mtindi huo, hakikisha unaupiga piga vizuri ukiwa kwenye bakuli kwa kutumia kijiko kama unavyo yapiga piga mayai unapotaka kuyakaanga, hadi utakapo ona mtindi umekuwa laini na hauna mabonge mabonge.

    Unaweza Pia Kusoma Hizi

    Leave a Review

    Your email address will not be published. Required fields are marked *


    The reCAPTCHA verification period has expired. Please reload the page.