Jarida la Mapishi

Mchuzi wa kuku wenye nazi

  • Maandalizi
    -
  • Kupika
    Dakika 35
  • Walaji
    4

Ingredients

    Directions

    Step1

    Chukua sufuria kubwa lenye mafuta ya kupikia na uliweke kwenye jiko lenye moto wa wastani, kisha acha mafuta yapate moto. Weka vitunguu maji kwenye hilo sufuria, kisha kaanga huku ukikoroga mara kwa mara kwa muda wa dakika 5, au hadi utakapo ona vimebadilika rangi na kuwa na rangi ya kahawia.

    Step2

    Weka majani ya mvuje, tangawizi, vitunguu swaumu, pamoja na nazi, kisha kaanga huku ukikoroga mara kwa mara kwa muda wa dakika 1.

    Step3

    Weka vipande vya nyama ya kuku, binzari ya manjano, pamoja na chumvi, kisha kaanga huku ukivigeuza vipande vya nyama ya kuku mara kwa mara kwa muda wa dakika 5, au hadi utakapo ona vimebadilika rangi na kuwa na rangi ya kahawia.

    Step4

    Mimina tui la nazi halafu koroga vizuri, kisha funika sufuria na uache ichemke kwa muda wa dakika 20, au hadi utakapo ona vipande vya nyama ya kuku vimeiva. Epua na upakue kwenye chombo safi, tayari kwa kula.

    Unaweza Pia Kusoma Hizi

    Leave a Review

    Your email address will not be published. Required fields are marked *


    The reCAPTCHA verification period has expired. Please reload the page.