Jarida la Mapishi

Mchuzi wa nyama ya mbuzi

Mchuzi wa nyama ya mbuzi | Jarida la Mapishi
  • Maandalizi
    -
  • Kupika
    Saa 1 Dk. 10
  • Walaji
    4

Mchuzi wa nyama ya mbuzi, ni kitoweo kitamu, ambacho hupikwa kwa kutumia nyama ya mbuzi, vitunguu maji, mtindi, pamoja na viungo vya aina mbalimbali. Mchuzi huu wafaa kula pamoja na wali au pilau. Fuata hatua zifuatazo, ili ujifunze jinsi ya kupika mchuzi huu wa nyama ya mbuzi.

Ingredients

    Directions

    Step1

    Chukua kontena dogo. Weka ndani ya hilo kontena, mtindi pamoja na zafarani, kisha changanya vizuri.

    Step2

    Chukua sufuria kubwa lenye mafuta ya kupikia na uliweke kwenye jiko lenye moto wa wastani, kisha acha mafuta yapate moto. Weka kwenye hilo sufuria, mdalasini, pilipili manga, iliki, majani ya mbei, karafuu, pamoja na binzari nyembamba, kisha kaanga huku ukikoroga mara kwa mara kwa muda wa dakika 2.

    Step3

    Weka vitunguu maji, kisha kaanga huku ukikoroga mara kwa mara kwa muda wa dakika 10 mpaka 12, au hadi utakapo ona vitunguu vimeiva.

    Step4

    Weka tangawizi, vitunguu swaumu, vipande vya nyama ya mbuzi, mbegu za giligilani, pamoja na chumvi, kisha kaanga huku ukikoroga mara kwa mara kwa muda wa dakika 10, au hadi utakapo ona vipande hivyo vimebadilika rangi na kuwa na rangi ya kahawia.

    Step5

    Mimina maji halafu koroga vizuri, kisha weka moto mkubwa na uache ichemke kwa muda wa dakika 5.

    Step6

    Punguza moto na uweke moto mdogo, kisha funika sufuria na uache iendelee kuchemka huku ukikoroga mara kwa mara kwa muda wa dakika 40, au hadi utakapo ona nyama imeiva.

    Step7

    Weka garam masala na ukoroge vizuri, halafu acha iendelee kuchemka kwa muda wa dakika 5 zaidi, kisha epua na uweke pembeni.

    Step8

    Weka mchanganyiko wa mtindi na zafarani, pamoja na majani ya giligilani, kisha koroga vizuri, tayari kwa kula.

    Conclusion

    Kabla ya kutumia mtindi huo, hakikisha unaupiga piga vizuri ukiwa kwenye bakuli kwa kutumia kijiko kama unavyo yapiga piga mayai unapotaka kuyakaanga, hadi utakapo ona mtindi umekuwa laini na hauna mabonge mabonge.

    Unaweza Pia Kusoma Hizi

    Leave a Review

    Your email address will not be published. Required fields are marked *


    The reCAPTCHA verification period has expired. Please reload the page.