Jarida la Mapishi

Muffins za tangawizi

Muffins za tangawizi | Jarida la Mapishi
  • Maandalizi
    Dakika 40
  • Kupika
    Dakika 20
  • Walaji
    12

Muffins za tangawizi, ni muffins tamu na rahisi kupika, ambazo hupikwa kwa kutumia viungo vya tangawizi, mdalasini pamoja karafuu. Unaweza kula muffins hizi wakati wowote ule upendao, pamoja na kinywaji chochote kile ukipendacho. Fuata hatua zifuatazo, ili ujifunze jinsi ya kupika muffins hizi za tangawizi.

Ingredients

    Directions

    Step1

    Chukua bakuli kubwa. Weka ndani ya hilo bakuli, siagi, mayai, buttermilk, tangawizi pamoja na vanilla extract, kisha changanya vizuri.

    Step2

    Weka light brown sugar, halafu endelea kuchanganya.

    Step3

    Weka unga wa ngano, chumvi, pamoja na baking powder, kisha changanya vizuri kwa kutumia mashine ya kuchanganyia (mixer), hadi utakapo ona mchanganyiko huo umechanganyika vyema na kuwa laini.

    Step4

    Chukua sufuria la kuoka muffins (muffins pan), lenye matundu 12 ya muffins, na uweke ndani ya hayo matundu karatasi za kuokea muffin (muffin papers). Chukua bakuli lenye mchanganyiko ulio changanya na mashine ya kuchanganyia, na umimine mchanganyiko huo kwenye sufuria la kuoka muffins.

    Step5

    Washa jiko la kuoka, na uweke joto la nyuzi 175° C, kisha acha jiko lipate moto. Jiko likishapata moto, weka sufuria la kuoka muffins ndani ya hilo jiko, na uoke kwa muda wa dakika 20, au hadi utakapo ona muffins zimeiva na kuwa na rangi ya kahawia.

    Step6

    Muffins zikisha iva, ziondoe kwenye jiko la kuoka, kisha ziweke pembeni ili zipoe, zikiwa bado ndani ya sufuria la kuoka muffins. Muffins zikishapoa, unaweza kuzitoa ndani ya sufuria la kuoka muffins, tayari kwa kula.

    Unaweza Pia Kusoma Hizi

    Leave a Review

    Your email address will not be published. Required fields are marked *


    The reCAPTCHA verification period has expired. Please reload the page.