-
Maandalizi-
-
KupikaDakika 40
-
Walaji4
Supu ya dengu, ni supu rahisi kupika na yenye afya, ambayo hupikwa kwa kutumia dengu, nyanya, tomato sauce, pamoja na viungo vya aina mbalimbali. Supu hii yafaa sana kunywa nyakati za jioni pamoja na chakula cha jioni. Fuata hatua zifuatazo, ili ujifunze jinsi ya kupika supu hii ya dengu.
Ingredients
Directions
Chukua kontena la ukubwa wa wastani. Weka maji, kisha roweka dengu ndani ya hilo kontena lenye maji kwa muda wa saa 24. Baada ya saa 24, mwaga maji yote yaliyomo kwenye kontena na kubakiwa na dengu peke yake.
Chukua sufuria kubwa. Weka kwenye hilo sufuria, dengu, vikombe 6 vya maji, mdalasini, iliki, tangawizi, vitunguu swaumu, pamoja na chumvi, kisha weka ichemke kwenye jiko lenye moto mkubwa.
Ukiona imeanza kuchemka, punguza moto na uweke moto mdogo, kisha funika sufuria na uache iendelee kuchemka kwa muda wa dakika 30, au hadi utakapo ona dengu zimeiva.
Ongeza moto na uweke moto mkubwa. Mimina tomato sauce, kisha pika mchanganyiko huo huku ukikoroga mara kwa mara kwa muda wa dakika 5.
Punguza moto na uweke moto wa mdogo, halafu endelea kupika mchanganyiko huo huku ukikoroga mara kwa mara kwa muda wa saa 1, kisha epua na uweke pembeni.
Chukua sufuria jingine kubwa lenye mafuta ya kupikia na uliweke kwenye jiko lenye moto wa wastani, kisha acha mafuta yapate moto. Weka tangawizi kwenye hilo sufuria, kisha kaanga huku ukikoroga mara kwa mara kwa kuda wa dakika 1, au hadi utakapo ona tangawizi imebadilika rangi na kuwa na rangi ya kahawia.
Weka binzari nyembamba, mbegu za giligilani, pamoja na binzari ya manjano, kisha kaanga huku ukikoroga mara kwa mara kwa muda wa sekunde 30.
Weka nyanya pamoja na majani ya giligilani, kisha pika mchanganyiko huo huku ukikoroga mara kwa mara, au hadi utakapo ona nyanya zimeiva na kuwa laini. Epua mchanganyiko huu na umimine kwenye sufuria lenye supu, kisha changanya vizuri, tayari kwa kula.
Leave a Review