Jarida la Mapishi

Viazi vyenye komamanga

Viazi vyenye komamanga | Jarida la Mapishi
  • Maandalizi
    -
  • Kupika
    Dakika 35
  • Walaji
    4

Viazi vyenye komamanga, ni chakula rahisi kupika chenye mchanganyiko wa ladha ya utamu na uchachu, ambacho hupikwa kwa kutumia viazi mviringo, mbegu za komamanga, pamoja na viungo vya aina mbalimbali. Viazi hivi vyafaa kula katika msimu wa sikukuu. Fuata hatua zifuatazo, ili ujifunze jinsi ya kupika viazi hivi vyenye komamanga.

Ingredients

    Directions

    Step1

    Chukua sufuria kubwa. Weka kwenye hilo sufuria viazi mviringo pamoja na maji, kisha chemsha kwenye jiko lenye moto wa wastani kwa muda wa dakika 20, au hadi utakapo ona vimeiva.

    Step2

    Epua na umwage maji yote yaliyomo kwenye sufuria na kubakiwa na viazi peke yake, kisha acha vipoe.

    Step3

    Menya maganda ya viazi hivyo, kisha vikate katika vipande vidogo vidogo.

    Step4

    Chukua kikaango kikubwa chenye mafuta ya kupikia na ukiweke kwenye jiko lenye moto wa wastani, kisha acha mafuta yapate moto. Weka kwenye hicho kikaango, mbegu za komamanga pamoja na mbegu za giligilani, kisha kaanga huku ukikoroga mara kwa mara kwa muda wa dakika 1.

    Step5

    Weka viazi ulivyo vichemsha pamoja na chumvi, kisha kaanga huku ukikoroga mara kwa mara kwa muda wa dakika 5 mpaka 7.

    Step6

    Weka majani ya giligilani pamoja na binzari nyembamba halafu kaanga huku ukikoroga mara kwa mara kwa muda wa dakika 3 mpaka 5, kisha epua na upakue kwenye chombo safi, tayari kwa kula.

    Unaweza Pia Kusoma Hizi

    Leave a Review

    Your email address will not be published. Required fields are marked *


    The reCAPTCHA verification period has expired. Please reload the page.