Jarida la Mapishi

Mboga ya kauliflawa

Mboga ya kauliflawa | Jarida la Mapishi
  • Maandalizi
    -
  • Kupika
    Dakika 40
  • Walaji
    4

Mboga ya kauliflawa, ni mboga tamu na rahisi kupika, ambayo hupikwa kwa kutumia kauliflawa, viazi mviringo, pamoja na viungo vya aina mbalimbali. Mboga hii yafaa kula pamoja na wali wa binzari ya manjano au chapati. Fuata hatua zifuatazo, ili ujifunze jinsi ya kupika mboga hii ya kauliflawa.

Ingredients

    Directions

    Step1

    Chukua sufuria kubwa lenye ½ kijiko cha chakula cha mafuta ya kupikia na uliweke kwenye jiko lenye moto wa wastani, kisha acha mafuta yapate moto. Weka viazi mviringo kwenye hilo sufuria, kisha kaanga huku ukikoroga mara kwa mara kwa muda wa dakika 5, au hadi utakapo ona vimebadilika rangi na kuwa na rangi ya kahawia. Ondoa viazi hivyo kwenye sufuria na uviweke pembeni kwenye kontena.

    Step2

    Weka ½ kijiko cha chakula cha mafuta ya kupikia yaliyobaki, kisha acha mafuta yapate moto. Weka kauliflawa, kisha kaanga huku ukikoroga mara kwa mara kwa muda wa dakika 5, au hadi utakapo ona imebadilika rangi na kuwa na rangi ya kahawia.

    Step3

    Weka viazi mviringo ulivyo vikaanga, kisha koroga vizuri.

    Step4

    Punguza moto na uweke moto mdogo. Weka tangawizi, binzari ya manjano, pamoja na chumvi, kisha funika sufuria na upike mchanganyiko huo huku ukikoroga mara kwa mara kwa muda wa dakika 15 mpaka 25, au hadi utakapo ona viazi na kauliflawa vimeiva na kuwa laini.

    Step5

    Weka majani ya giligilani, kisha pika mchanganyiko huo huku ukikoroga mara kwa mara kwa muda wa dakika 5.

    Step6

    Nyunyizia garam masala halafu koroga vizuri, kisha epua na upakue kwenye chombo safi, tayari kwa kula.

    Unaweza Pia Kusoma Hizi

    Leave a Review

    Your email address will not be published. Required fields are marked *


    The reCAPTCHA verification period has expired. Please reload the page.