Jarida la Mapishi

Mchuzi wa maboga

Mchuzi wa maboga | Jarida la Mapishi
  • Maandalizi
    -
  • Kupika
    Dakika 30
  • Walaji
    4

Mchuzi wa maboga, ni mchuzi wenye ladha nzuri na rahisi kupika, ambao hupikwa kwa kutumia maboga, mbaazi, choroko, tui la nazi, pamoja na viungo vya aina mbalimbali. Mchuzi huu wafaa kula pamoja na wali mweupe, wali wa brown, mkate au chapati. Fuata hatua zifuatazo, ili ujifunze jinsi ya kupika mchuzi huu wa maboga.

Ingredients

    Directions

    Step1

    Chukua sufuria kubwa. Weka kwenye hilo sufuria, maboga, mbaazi, binzari ya manjano, chumvi, pamoja na maji halafu koroga vizuri, kisha weka ichemke kwenye jiko lenye moto mkubwa.

    Step2

    Ukiona imeanza kuchemka, punguza moto na uweke moto wa wastani, kisha funika sufuria na uache iendelee kuchemka kwa muda wa dakika 10 mpaka 15, au hadi utakapo ona maboga pamoja na mbaazi vimeiva.

    Step3

    Weka nazi pamoja na binzari nyembamba, halafu koroga vizuri, kisha acha iendelee kuchemka kwa muda wa dakika 10 mpaka 12, au hadi utakapo ona maji yamekaribia kukauka. Epua mchanganyiko huu na umimine kwenye kontena.

    Step4

    Chukua sufuria dogo lenye mafuta ya kupikia na uliweke kwenye jiko lenye moto wa wastani, kisha acha mafuta yapate moto. Weka choroko kwenye hilo sufuria, kisha kaanga huku ukikoroga mara kwa mara kwa muda wa sekunde 30, au hadi utakapo ona zimebadilika rangi na kuwa na rangi ya kahawia.

    Step5

    Weka mbegu za haradali pamoja na majani ya mvuje, kisha koroga vizuri. Epua mchanganyiko huu na umimine kwenye kontena lenye mchanganyiko wa maboga, kisha changanya vizuri, tayari kwa kula.

    Unaweza Pia Kusoma Hizi

    Leave a Review

    Your email address will not be published. Required fields are marked *


    The reCAPTCHA verification period has expired. Please reload the page.