Jarida la Mapishi

Mchuzi wa nyama ya ng’ombe

Mchuzi wa nyama ya ng’ombe | Jarida la Mapishi
  • Maandalizi
    -
  • Kupika
    Saa 1 Dk. 55
  • Walaji
    4

Mchuzi wa nyama ya ng’ombe, ni kitoweo chenye ladha na harufu nzuri, ambacho hupikwa kwa kutumia nyama ya ng’ombe, vitunguu maji, nyanya, mtindi, pamoja na viungo. Fuata hatua zifuatazo, ili ujifunze jinsi ya kupika mchuzi huu wa nyama ya ng’ombe.

Ingredients

    Directions

    Step1

    Chukua sufuria kubwa lenye mafuta ya kupikia na uliweke kwenye jiko lenye moto mkubwa, kisha acha mafuta yapate moto. Weka vitunguu maji kwenye hilo sufuria, kisha kaanga huku ukikoroga mara kwa mara kwa muda 3 mpaka 5.

    Step2

    Punguza moto na uweke moto wa wastani, kisha endelea kukaanga huku ukikoroga mara kwa mara kwa muda wa dakika 12, au hadi utakapo ona vitunguu vimebadilika rangi na kuwa na rangi ya kahawia.

    Step3

    Weka tangawizi pamoja na vitunguu swaumu, kisha kaanga huku ukikoroga mara kwa mara kwa muda wa dakika 1.

    Step4

    Weka nyanya, kisha pika mchanganyiko huo huku ukikoroga mara kwa mara kwa muda wa dakika 5, au hadi utakapo ona mchuzi umekuwa mzito.

    Step5

    Weka mbegu za giligilani, garam masala, binzari nyembamba, pamoja na binzari ya manjano, kisha pika mchanganyiko huo huku ukikoroga mara kwa mara kwa muda wa sekunde 30.

    Step6

    Ongeza moto na uweke moto mkubwa. Weka nyama pamoja na chumvi, kisha pika mchanganyiko huo huku ukikoroga mara kwa mara kwa muda wa dakika 3 mpaka 5.

    Step7

    Punguza moto na uweke moto wa wastani, kisha endelea kupika mchanganyiko huo huku ukikoroga mara kwa mara kwa muda wa dakika 15 mpaka 20, au hadi utakapo ona nyama imebadilika rangi na kuwa na rangi ya kahawia.

    Step8

    Mimina mtindi taratibu huku ukikoroga, kisha acha ichemke kwa muda wa dakika 5, au hadi utakapo ona mtindi umekauka.

    Step9

    Weka maji halafu koroga vizuri, kisha funika sufuria na uache ichemke kwa muda wa dakika 45 mpaka 55, au hadi utakapo ona nyama imeiva na mchuzi umekuwa mzito.

    Step10

    Weka majani ya uwatu halafu koroga vizuri, kisha acha ichemke kwa muda wa dakika 5 zaidi. Epua na upakue kwenye chombo safi, tayari kwa kula.

    Conclusion

    Kabla ya kutumia mtindi huo, hakikisha unaupiga piga vizuri ukiwa kwenye bakuli kwa kutumia kijiko kama unavyo yapiga piga mayai unapotaka kuyakaanga, hadi utakapo ona mtindi umekuwa laini na hauna mabonge mabonge.

    Unaweza Pia Kusoma Hizi

    Leave a Review

    Your email address will not be published. Required fields are marked *


    The reCAPTCHA verification period has expired. Please reload the page.